Find Us Online At
iBookstore
Android app on Google Play
Like Us
A programme by
Utafutaji wa Chanzo cha Ulimwengu Umeanza
13 March 2013

Leo hii telescope mpya iitwayo ALMA imefungua macho yake. Telescope hii ni kubwa kuliko zote hapa Duniani; imetengenezwa na antenna 54 za madishi yenye mita 12 (sawa sawa na jengo lenye ghorofa nne!) na pia antenna ndogo kumi na mbili zenye mita 7. Madishi haya 66 yatakuwa yanafanya kazi kwa pamoja ili kufanya telescope yenye nguvu katika uso wa Dunia! ALMA inaweza kuona mwanga kutoka katika vitu vilivyo mbali sana katika ulimwengu, ili kutuonyesha taarifa ambazo hazijawahi kuonekana za mwanzo wa ulimwengu. Picha hii ya kupendeza inaonyesha Telescope ya ALMA ilivyotapakaa kukatiza jangwa la Atacama nchini Chile. 

Wakati Ulimwengu ulipokuwa mchanga, ulikuwa umejawa na ukungu mzito wa gesi ya haidrojeni. Hii ilifanya iwe ngumu kuuchunguza kwa kutumia telescope zinazotumia mwanga wa kawaida unaonekanao kwa macho. Lakini ALMA ina jicho la pekee ambalo linaweza kuangalia ulimwengu katika mwanga tofauti ujulikanao kama ‘mwanga wa radio’. Hii itaifanya telescope hii iweze kupenya katika ukungu na kuonyesha siri zilizijificha humo kwa mara ya kwanza. 

ALMA pia inaweza kutupa ufahamu wa vitu vyenye ubaridi sana katika ulimwengu. Itaweza kupenya katika magimba meusi ya gesi na vumbi ambayo yana jotoridi lililopo chini kidogo ya absolute sifuri — ambao ni ubaridi wa chini kabisi unaoweza kufikiwa (-273 °C). Ubaridi unaoweza kukaribia ubaridi wa kutembea kusini na kuelekea kizio cha kusini cha Dunia! Tunategemea kuvumbua sayari mpya ambazo zinazunguka majua mengine ya mbali na nyota mpya zinazozaliwa katika magimba manene. 

Kama unataka kuwa wa kwanza kujua siri zinazovumbuliwa na ALMA kuhusiana na chanzo cha ulimwengu wetu, basi hakikisha unasoma space scoops katika miezi inayofuta! 

Dokezo

ALMA imetengenezwa katika mlima wenye mwinuko wa mita 5000 uliopo katika jangwa la Atacama, Chile. Moja kati ya sehemu kame zaidi katika Dunia! Mwinuko huu mkubwa na ukame uliopo katika eneo hilo unamaanisha kuwa kuna kiasi kidogo sana cha mawingu kinachoweza kuingilia uchunguzi. Lakini katika mita 5000 hewa ni ndogo sana, hivyo binadamu hawakai sana katika eneo hilo. 

Share:

More news
12 October 2020
1 October 2020
16 September 2020
14 September 2020
10 September 2020

Images

The Search for our Cosmic Origins Begins
The Search for our Cosmic Origins Begins

Printer-friendly

PDF File
1.1 MB